“MUNGU KWETU SISI
NI KIMBILIO NA NGUVU
MSAADA UTAKAO ONEKANA TELE
WAKATI WA MATESO”
BARAKA. A. KAMINYOGE
“MUNGU KWETU SISIS
NI KIMBILIO NA NGUVU
MSAADA UTAKAO ONEKANA TELE
WAKATI WA MATESO”
TOLEO LA1: MARCH 2018
Haki zote zimehifadhiwa
BARAKA .A.KAMINYOGE
0758431829,0683903106
DODOMA-TANZANIA
facebook:Baraka andendekisye
email:bandendekisye@gmail.com
youtube:bak man
YALIYOMO
KIMBILIO LA WATAKATIFU WALIOPO DUNIANI.
Kimbilio ni mahali
palipo na msaada baada ya kupita katika eneo ambalo ni gumu na kushindwa
kujiokoa au kujilinda kwa namna yoyote na hapo unapata mahali pa kukimbilia na
kusaidiwa iwe ni kiroho au kimwili.
Kwa mfano
mvua ikiwa inanyesha watu hukumbili mahali penye nyumba ambapo wana amini
hawawezi kulowana na kuathirika na mvua hiyo katika afya zao. Hivyo hujiokoa
afya zao pamoja na mali walizo taka zisilowane na maji ya mvua, kilicho
wasaidia ni kimbilio nyumba.
Mfano
mwingine wa kimbilio ni huu , Jua linapo kuwa kali mtu yupo njiani kweupe kama
jangwani, huwa anateseka na jua sana na mahali pa kukimbilia hakuna inapotokea
ameona mti wenye kinvuli mara moja huenda kupumnzika kwa muda ili aendelee na
safari tena, wengine japo wana hraka wakifika kwenye mti namna hiyo hutamani
wasiondoke hufanya mti kuwa ni kimbilio. Nina amini umeelewa maana ya
kimbilio ni mahali pa kujificha usipatwe na baya na ni mahali pa kupata msaada
wako.
Watakatifu – ni wanadamu waliopo duniani walio
amua kuacha dhambi kabisa na kuwa balozi wa mungu duniani yani muwakilishi wa
mungu duniani.
Watakatifu wa mungu huishi maisha ya toba
,huishi maisha ya wokovu,huishi maisha ya imani,hiushi maisha ya upendo, huishi
maisha neno la kristo,huishi kwa kanuni za mungu,huishi kwa kuongozwa na Roho
wa mungu,huishi maisha ya kutaka kufikia kimo cha kristo na kutenda kama kristo
ila kwa nguvu ya kristo yesu mwenyewe.
Duniani- ni
mahali watu walio na mwili wa damu na nyama na viumbe vingine hai vinapatikana
(ulimwengu). Katika dunia yapo mambo mengi mema na mabaya ambayo mwanadamu
huyaona na kuyafanya ila mtakatifu wa mungu hafanyi yaliyo nje ya mungu.
Atendaye kinyume cha mungu ni Yule asiye mtakatifu/ambaye hajamjua kristo.
Duniani hakuna kuishi milele ni mahali pa
kupita tukitoka duniani kuna eneo tutaelekea tena kuishi milele ambako ni
mbinguni na jehanamu watenda mabaya wataenda jehanamu watakatifu wa Mungu
watakwenda mbinguni.
Ni imani
yangu kuwa kichwa cha somo umekielewa vema na ni kwa msaada wa Roho mtakatifu
kabisa, kinachosema KIMBILIO LA
WATAKATIFU WALIOPO DUNIANI.
Zaburi 46: 1 Mungu
kwetu sisi ni kimbilio na nguvu, Msaada utakaoonekana tele wakati wa mateso. 2 Kwa hiyo hatutaogopa ijapobadilika nchi, Ijapotetemeka milima moyoni mwa bahari.
Mambo yanayopatikana hapa
i.
Mungu
kwetu sisi
ii.
Ni
kimbilio
iii.
Ni
nguvu
iv.
Msaada
unao onekanatele.
v.
Wakati
wa mateso
vi.
Hatutaogopa
ijapo badilika nchi
vii.
Hatutaogopa
ijapo tetemeka milima moyoni mwa bahari.
i)MUNGU KWETU SISI
Hapa biblia inapo mzungumzia mungu aliye
muumba mbingu na nci inaonyesha kuwa ipo miungu mingine ndio maana ameonyesha umiliki wa “mungu kwetu sisi” wana mtambulisha mungu wao kuwa
huyo mungu ni mungu wa namna gani na ana uwezo gani na kuwa huyo mungu ni
tofauti kabisa ni miungu mingine ambayo mungu amewakataza waatakatifu wasi
iabudu, kutoka20:4 Usijifanyie sanamu ya kuchonga,
wala mfano wa kitu cho chote kilicho juu mbinguni, wala kilicho chini duniani,
wala kilicho majini chini ya dunia. 5 Usivisujudie wala kuvitumikia; kwa kuwa mimi, Bwana, Mungu wako, ni Mungu mwenye wivu; nawapatiliza wana maovu ya baba zao, hata kizazi cha tatu na cha nne cha wanichukiao,
6 nami nawarehemu maelfu elfu wanipendao, na kuzishika amri zangu.
Kwahiyo biblia
inaonyesha kuwa mtakatifu wa mungu aliye hai ndiye watakatifu wanamwamini huyo
na hawana mungu mwingine ila yeye ndio maana mungu amewakataza kumwabudu
mwingine yeyote. Mimi na wewe kwakuwa tumempokea kristo ndani mwetu ni
watakatifu na mungu aliye umba mbingu na nchi ndiye mungu kwetu sisi.
Huyu mungu kwetu sisis watakatifu tukimwita
anaitika, tukimwomba anatupa tuombacho, tukibisha mlangoni anafungua, hujibu
sawasawa nakuomba kwetu kwa mapenzi yake, hutu ponya magonjwa,hutusaidia kwenye
shida,hutusamehe maovu, hutuinua toka chini kwenda juu, nafsi iliyo inama
huiinua tena.
Amua ndani ya moyo wako kumwamini huyu Mungu
mwokozi awe wako na ukiwa na shida yoyote ipeleke kwake naye atafanya.
Mwandishi zaburi alipoona amemtumia mungu na mungu akamjibu akasema Zaburi 46: 1 Mungu kwetu sisi ni kimbilio na nguvu, Msaada
utakaoonekana tele wakati wa mateso. 2 Kwa hiyo hatutaogopa ijapobadilika nchi, Ijapotetemeka milima moyoni mwa bahari.
Maana alimwona wazi wazi , namimi nina amuru imani ipandwe ndani mwako ya kumwamini huyu bwana mwenye nguvu hodari wa vita akupigania katika kila hatua ufanyayo kwa jina layesu ,yoshua24: 14 Basi sasa mcheni Bwana, mkamtumikie kwa unyofu wa moyo na kwa kweli; na kuiweka mbali miungu ambayo baba zenu waliitumikia ng'ambo ya Mto, na huko Misri; mkamtumikie yeye Bwana.
15 Nanyi kama mkiona ni vibaya kumtumikia Bwana, chagueni hivi leo mtakayemtumikia; kwamba ni miungu ile ambayo baba zenu waliitumikia ng'ambo ya Mto, au kwamba ni miungu ya wale Waamori ambao mnakaa katika nchi yao; lakini mimi na nyumba yangu tutamtumikia Bwana.
amen.
iI) MUNGU KWETU NI
KIMBILIO
Ukiokoka mungu anakuwa kimbilio kwako maana huna mkuu
mwingine zaidi yake yeye mungu aliye umba mbingu na nchi.
Mtoto ana amini kuwa yeyote akimpiga akimwambia
baba au mama au mlezi yeyote hufanyika kuwa msaada ndio maana anakimbilia kwake
, hivyo tunaye baba wa kiroho ambaye ni mungu tukimwambia haja zetu yeye
husikia na kufanyika kuwa msaada kwetu. Usiangaike kuwa ni miungu mingine
unapoteza muda maana yupo mungu mkuu mungu wa kweli asiye shindwa na lolote
amesema tuombe kwake lolote atatenda yote yohana15:
6 Ninyi mkikaa ndani yangu, na
maneno yangu yakikaa ndani yenu, ombeni mtakalo lote nanyi mtatendewa. 7 Hivyo hutukuzwa Baba yangu, kwa vile mzaavyo sana; nanyi mtakuwa wanafunzi wangu.
Iambie nafsi yako na moyo wako
umpokee mungu ndani yako ili awe kimbilio kwako na akupe kile utakacho sawasawa
na kuamini kwako,
hii nafasi ya mungu kuwa kimbilio kwako sio ya kawaida maana wako wanao kwenda
kwa waganga lakini nako hapajawa kimbilio la matatizo yao kabisa , wamekimbilia
mizimu wamebaki wakiangaika na kuteseka lakini walipo amua kukimbilia jina la
yesu wakawa salama.
Omba maombi haya mwambie bwana yesu fanyika
kuwa kimbilio kwangu na uwe karibu nami niombapo lolote unipe kwa mapenzi yako
katika jina la yesu aimeni. Yohana14:12 Nanyi mkiomba lo lote kwa jina langu, hilo
nitalifanya, ili Baba atukuzwe ndani ya Mwana. 13 Mkiniomba neno lo lote kwa jina langu, nitalifanya.
ii)Mungu kwetu ni nguvu
Mfanye
mungu kuwa ni nguvu kwako ili uweze kuishi maisha ya utakatifu
jinyenyekeze chini ya mungu ili msaada wa mungu usikupite kwa njia ya
utakatifu. Ukimtegemea mungu kuwa nguvu kwako unao uwezo wa kushinda kila
jaribu kil jambo ambalo wengine wanashindwa kufanya walio mtegemea mwanadamu
maana imeandikwa yeremia17: 5 Bwana asema hivi, Amelaaniwa mtu yule
amtegemeaye mwanadamu, Amfanyaye mwanadamu kuwa kinga yake Na moyoni mwake
amemwacha Bwana. 6 Maana atakuwa kama fukara nyikani, Hataona yatakapotokea mema; Bali atakaa jangwani palipo ukame, Katika nchi ya chumvi isiyokaliwa na watu.
7 Amebarikiwa mtu yule anayemtegemea Bwana, Ambaye Bwana ni tumaini lake.
iv)Msaada unao
onekanatele
Mungu ni msaada kwako ukimtegemea na
kumwamini, amua ndani ya moyo wako mungu awe msaada kwako tangu leo ili uishi
maisha ya kumpendeza yeye na uwe salama maada kila utakalo kwa msaada wake
litafanyika usitumie akili yako muda mrefu mwambie bwana nae atafanya kwa
haraka mno maana msaada huwa huchelewi . tena amewekeka msaada tele maana yake
msaada huo unasubiria wewe uitaji ili utumike maana umezidi.
Baba katika jina la yesu kristo
ninaomba kila ninapo hitaji msaada kutoka kwako iwe ni
fedha,mali,gari,nyumba,afya,imani,wokovu nipate kwa jina la yesu ameni. zaburi:60: 12 Kwa
msaada wa Mungu tutatenda makuu, Maana Yeye atawakanyaga watesi wetu.
vi)Wakati wa mateso
10 Kwa maana wangawa kama miiba iliyotatana, na kunyweshwa kana kwamba ni katika kunywa kwao, wataliwa kabisa kama mabua makavu.
i.
Hatutaogopa
ijapo badilika nchi
Mtu aliye
okoka anao ulinzi wa bwana hata yangetokea magumu yakutisha yeye haogopi
kwahiyo nakutia moyo usiogope usiogope isaya41:
10 usiogope, kwa maana mimi ni pamoja nawe; usifadhaike, kwa
maana mimi ni Mungu wako; nitakutia nguvu, naam, nitakusaidia, naam,
nitakushika kwa mkono wa kuume wa haki yangu. Mungu akutie ujasiri katika kila jambo ufanyalo usiogope majaribu maana
yapo kwa kadiri ya imani yako wala huta anguka kabisa wala hayata kushinda
maana bwana ni kimbilio lako na ni uzima wako katika jina la yesu roho ya hofu
naiondoa kwako.
No comments:
Post a Comment